INSIDE INAPATIKANA MADUKANI

FILAMU YA JADA ITAKUWA SOKONI 19.02.2015

JADA IPO SOKONI

JADA IPO SOKONI

Monday, December 28, 2015

Picha: Diamond, Zari, AY, Esma, Queen Darleen Wakifurahia Holiday Ufukweni.

Zari, Diamond, Queen Darleen, Esma Platnumz na management ya Diamond waliamua kufanya mapumziko ya holiday katika ufukwe wa bahari ya hindi huku pia wakipanda yatch

Odama, AY Na Bob Junior Kukinukisha Kesho.

Odama atakuwa na special appearance katika party itakayofanyika kesho ukumbi wa Rhapsodys..

Nazingatia Ubora Wa Filamu Kwanza Pesa Baadaye. : JB

‘’Wakati mwingine nakuwa kama kichaa nikitengeneza movie zangu siangalii namna ambavyo nitapata faida kubwa,naangalia jinsi ambavyo naweza kutengeneza kitu kizuri,naaamini katika maisha kuacha historia bora kuliko kitu chochote,hadi sasa nimeshatengeneza zaidi ya filamu 37 kutoka kwenye kampuni yangu ya Jerusalem,’’alisema JB.
‘’Pesa Napata lakini kumbukumbu yangu ni filamu zile ambazo watu wameangalia wakikuona na kukuita yale majina kama Erik Ford,Dj Ben,Danija,Mzee wa Swaga ndiyo majina yanayobaki kuwa kumbukumbu kwa sababu waliona nilichokifanya,sitajali nimetumia mill.100 au mia mbili kwenye local movies hata kama haitorudi ili mradi filamu iwe nzuri,’’alisema JB.
Cloudsfm.com

Jokate Na Wema Katika Show Ya Ali Kiba.

Juzi Ali Kiba Alikuwa na show ya kuwaaga mashabiki wake kwa kumaliza mwaka vziuri katika ukumbi wa Escape One Mikocheni. Miongoni mwa walihudhuria hiyo show ni Wema Sepetu na Jokate. Angalia picha ..

Sunday, December 27, 2015

Mama Lulu Agoma Lulu Kuondoka Nyumbani.

Marufuku! Mama mzazi wa staa wa Bongo Movies, Elizabeth Michael ‘Lulu’, Lucresia Karugila ametia ngumu mwanaye huyo kuondoka nyumbani kwake na kwenda kuishi peke yake kwa kuwa bado anahitaji zaidi kufuata maadili yake.

Riyama Ally Na Flora Mvungi Wakabana Koo Kukata Nyonga.

STAA wa filamu Bongo, Flora Mvungi na shostito wake, Riyama Ally juzikati walijikuta wakigeuka kivutio ukumbini baada ya kufunikana kwa kuzikata nyonga bila aibu kwenye hafla ya kumpongeza mtoto wa Flora, Tanzanite Hamis kuchaguliwa kuwa balozi wa duka la kuuza nguo.

Zamaradi Mketema Kumuingiza Mama Diamond Bongo Movie.

Kufuatia uwezo mkubwa aliouonyesha Mama mzazi wa staa wa Bongo Fleva, Diamond Platinum, Sanura Kasim kwenye kipande cha video ya wimbo mpya wa diamond , utanimpenda ambapo mama huyo ameigiza kwa kuuvaa uhusika wa mama mwenye maisha magumu ambaye anatafuta msaada akiwa na mtoto mgongoni kitu ambacho kimeshika hisia za watazamaji wengi na wengi kumuona kama ni mama mwenye uwezo mkubwa wakuigiza, mmoja wapo ni mtangazaji na muuandaaji wa filamu hapa Bongo, Zamaradi Mtetema ambaye amekiona kipaji cha mama huyu na kuahidi kumtafuta ili wafanye kazi.

Lady Jaydee Ahamia Ujerumani ?

MOYONI nina majonzi, sina tofauti na mpofu! Judith Wambura Mbibo ‘Jide’ au ‘Lady Jaydee’ kwa sasa hana makazi maalum Bongo, amehamishia makazi na shughuli zake katika ardhi ya ‘Kansela’ wa Ujerumani, Angelina Merkel kwenye Jiji la Born.
Katika mazungumzo yake na mwandishi wetu kwa njia ya simu, Jumatatu ya wiki hii, Jide ambaye alidai kwa sasa yupo nchini kwa Sikukuu ya Krismasi (kesho), alisema sababu zilizomfanya akapige kambi nchini humo ni kuchoshwa na maneno ya watu ambao kazi zao ni kutazama nani kafikwa na baya ili waeneze sumu ya maneno.

Tuesday, December 22, 2015

Wema Sepetu Kuonekana Akipika Mahanjumati Wiki Hii.

“This week ntakua Jikoni na my Dada Marion- Alhamis 24th December at 7pm Dstv Maisha Magic Bongo (Channel 160). An Exclusive Interview and Cooking section”-Wema ameandika kwenye ukurasa wake mtandaoni baada ya kutupia picha hizi akiwa jikoni.

Aunty Ezekiel Na Moze Iyobo Kupata Mtoto Mwingine.

Staa maarufu wa filamu Bongo, Aunty Ezekiel amefungua kinywa chake na kusema kuwa kwa sasa yuko kwenye mchakato wa kumtafuta mdogo wake na Cookie kwa kuwa hataki kukaa muda mrefu ili kupata mtoto mwingine.
Akizungumza na mwandishi wa habari hii hivi karibuni Aunty,alisema kuwa ameamua kufanya hivyo kwa kuwa anaona kuzaa mapema na kumaliza ndiyo poa ili aweze kuendelea na kazi zake vizuri kuliko kukaa muda mrefu halafu ndiyo ubebe ujauzito tena.

TANESCO Wataja Gharama Wanazomdai Wema Sepetu.

Shirika la Umeme nchini (TANESCO) limemkaba koo staa maarufu wa Bongo Movies , Wema Sepetu baada ya kubainika kutumia nishati ya umeme kwa njia zisizo halali.
Hivi karibuni TANESCO walifanya ziara ya kushtukiza kwenye nyumba yake na kubaini kuwa muigizaji huyo anatumia umeme wao bure!

Wasanii Wajitokeza Kugombea Nafasi Za Uongozi.

MCHUANO mkali katika kinyang’anyiro cha kugombea nafasi ya mwenyekiti wa chama cha waigizaji Taifa (TDFAA) huku wasanii wenye ushawishi kwa wasanii wenzao wakijitokeza kuchukua fomu za kugombea nafasi hiyo anasema katibu Twiza.
Jimmy Mafufu akichukua fomu ya kugombea kutoka kwa katibu wa TDFAA Twiza Mbarouk .
Jimmy Mafufu akichukua fomu ya kugombea kutoka kwa katibu wa TDFAA Twiza Mbarouk .
“Mchuano ni mkali kila mhusika amepanga kuwa ni mshindi katika kinyang’anyiro cha kugombea nafasi ya uenyekiti Kitaifa kwa chama cha Waigizaji, hadi sasa ni zaidi ya wasanii wane wameshachukua fomu za kugombea,”anasema Twiza.

Wasanii Tufanye Na Biashara Nyingine Tujikwamue Kiuchumi: Ire Uwoya

MKALI wa filamu nchini, Irene Uwoya, amewataka wasanii wenzake hasa wanawake kujituma katika kazi nyingine kama vile biashara ili kuweza kujikomboa kiuchumi
Irene amesema wasanii wengi wanategemea sanaa ili kuweza kuendesha maisha yao, lakini wanatakiwa kufanya mambo mengi ili kuweza kujiingizia kipato.

Lulu Haishi Vituko, Angalia Alichoandika.

Hapa na Pale: Kupitia ukurasa wake kwenye mtandao picha wa Instagram staa mrembo wa Bongo Movies, Elizabeth Michael ‘Lulu’ amewaacha watu hoi baada ya kubandika picha hiyo hapo chini ikimuonyesha yeye na baba yake mzazi ‘Mzee Michael’ na kummwagia sifa baba yake huku akiomba dua aje kuzaa mtoto atakaye fanana na baba yake (Mzee Michael) kitendo ambacho kila shabiki yake mtandaoni alikuwa na yake ya kusema.

Friday, December 18, 2015

Picha Kutoka Birthday Ya Faiza Ally.

Jana ilikuwa birthday ya Faiza Ally ambayo ilihudhuriwa na mastaa kadhaa wa filamu nchini. Faiza pia alivaa gauni la harusi na shela. Hizi ni picha...

Chungu Cha 3 Ya Wema Sepetu Na JB Yapokelewa Vizuri Sokoni.

“Kwanza nawashukuru sana sana kwa kuipokea vyema filamu ya Chungu cha tatu. …pili nawaomba radhi wote ambao jana walikosa nakala zao kwani iliisha tena…lakini leo ipo madukani baada ya mimi mwenyewe kukesha kiwandani nikihakikisha oda zote watu wanapata..mikoani pia sehemu ambazo ziliisha leo zipo…nimepata habari za watu wanaouza feki tayari baadhi yao wako ndani…asanteni..” alisema JB kwenye page yake. Filamu ya Chungu Cha Tatu imechezwa na JB na Wema Sepetu kama wahusika wakuu

Picha Kutoka Zari All White Party 2015 Nchini Uganda.

Zari All White Party nchini Uganda imefanyika jana, Ingawa Diamond alikuwa Uganda pia hakuweza kuhudhuria kutokana na kuwa na show pia. Ila aliyewahi kuwa mume wa Zari yaani Ivan Semwanga alihudhuria. hizi ni picha..
Zari All White Ciroc Party
Zari All White Ciroc Party

Tuesday, December 15, 2015

Shamsa Ford Awatolea Uvivu Waliomnanga Kwa Kuvaa Nguo Fuoi.

"Maisha yangu hayawahusu. Ukiona hufulahishwi na chochote toka kwangu ni unfollow. Hukulazimishwa kunifollow. Yaani kuniona kwenye movie ndo mnajifanya mnanijua mpaka mnipangie maisha ya kuishi.sikilizeni nitavaa nitavyojisikia mm hata nikiamua kukaa uchi kabisaa ni mm na wala hayakuhusu. Ww subili movie Itoke ndo unikosoe. Mnaboa sana. Hebu walekebisheni ndugu zenu wanaovaa madila mchana usiku ni vyangudoa..." ameandika Shamsa Ford baada ya baadhi ya watu kumtukana kwa nguo fupi aliyoivaa akiwa beach na mwanae......

Monday, December 14, 2015

Lulu, Monalisa, Richie Wachaguliwa Tuzo Za Africa magic Viewer's Choice Awards 2016.

Filamu 4 za kitanzania zimechaguliwa katika katika tuzo za Africa Magic Viewers Choice Awards 2016 zitakazofanyika nchini Nigeria mwezi wa tatu. Filamu hizo ni Kitendawili iliyoigizwa Single Mtambalike Richie na Irene Veda, Mapenzi Ya Mungu iliyoigizwa na Lulu, Daddy's Wedding iliyoigizwa na Monalisa na Mpango Mbaya zote zikiwania best East African Film. Huku Kitendawili pia ikichaguliwa kuwania best Indigenous Film(Swahili). Ili kuwapigia kura wasanii hawa angalia maelezo hapo chini....

Kingwendu Apata Deal La Uigizaji Nchini Ujerumani.

Msanii maarufu wa vichekesho na maigizo nchini Kingwendu siku chache zilizopita ameenda nchini Ujerumani kwa ajili ya masuala ya uigizaji. Kingwendu ambaye aligombea ubunge hivi karibuni na kuukosa kabala hajaondoka alisema kuwa mwaka ujao wameamua wasanii wa vichekesho waitangaze tasnia ya filamu kimataifa baada ya waigizaji serious kushindwa kuiendeleza alipoishia Kanumba.

Tuesday, December 8, 2015

Shaa Na Vanessa Mdee Wakerwa na Baadhi Ya Mashabiki Kuwalinganisha Na Kuwashindanisha

Mastaa wa muziki wa kisazi kipya Vanessa Mdee na Shaa kwa nyakati tofauti wakizungumza katika kipindi cha Planet Bongo wameonekana kukerwa na baadhi ya mashabiki kuwashindanisha wao kwa wao wakisema kuwa sio vizuri kwasababu inaleta uhasama baina ya wasanii wa ndani wakati kila mmoja ana nafasi na mchango wake katika sanaa ya Tanzania. Shaa alisema ni heri mashabiki wawashindanishe na wasanii wa nje maana wasanii wa ndani kwa ndani haileti maana

Wema Sepetu Kufanya Makubwa Zaidi.

"I think This should be my Colour ya Lipstick wen it comes to my Brand Kiss..... Naipenda coz it jus makes me feel good nikiipaka.... For a very long time nimekuwa nikitaka sana kuwa na kitu kitacho carry jina langu la Wema Sepetu... I thought of perfume at first ila huko nikahisi ni parefu sana but inshallah hakunaga kubwa ukimtanguliza Mungu katika jambo lako na haswa likiwa jambo la kheri.... but sababu napenda urembo nikawaza nifanye kitu kiatakacho reflect kwenye urembo na wazo la kwanza lililonijia katika kichwa ni My Kissable Lips..... 🙈🙊 So hapo hapo nikasema Why nat make a Lipstick kuzifanya kissable lips zangu zizidi kuvutia na ziweze kuwafanya na my fellow sisters pia wawe na muonekano mzuri..... Tumeanza na Lipstick jamani... Mdogo mdogo ndo mwendo.... Inshallah kale ka makeup box ketu ambacho wadada hatukosagi kwenye handbag zetu katakuwa na virutubisho vyote vya uso wako kwanzia foundation mpaka wanja vikiwa na jina la your sweetheart Wema Sepetu..... Tuombeane Kheri and like I said hakunaga kubwa kwa Allah.." Ameandika Wema kwenye instagram

Tanesco Wagundua Wizi Wa Umeme Nyumbani Kwa Wema Sepetu, Idris Sultan Ndani Ya Nyumba

Katika Pitapita zao leo kufanya majukumu yao ya kikazi Tanesco walipita mitaa ya Makumbusho kukagua nyumba ikiwemo ya Wema Sepetu ambapo habari zinasema kuwa Tanesco walikuta kuwa umeme unatumika lakini hausomi kwenye mita yaani haulipiwi. Pia Idris Sultan ambaye ni mtu wa karibu na Wema alikuwa ndani ya nyumba akijaribu kuwasihi Tanesco wasikate umeme. Wema Bado kuzungumzia suala hilo. Picha hapo chini ni Idris akiwa nyumbani kwa Wema wakati Tanesco wakifanya yao ambapo pia waandishi wa habari walikuwepo.

Odama Aingia Mzigoni Kushuti Filamu Mpya.

Star wa filamu nchini Odama Jennifer Kyaka ameingia location tayari kuanza kushuti filamu yake mpya baada ya kimya cha muda kidogo.

Quick Racka Akiri Kuwa Katika Penzi Na Kajala

Msanii wa BongoFlava Quick Racka amekiri kuwa na uhusiano na Kajala Masanja licha ya huko nyuma wote kutokuwa tayari kuzungumzia uvumi huo ambao ulichukuwa headline za magazeti. Hata hivyo akizungumza na Clouds Fm Quick Racka aliulizwa kama swali flani la kimitego hivi kuwa ni kweli wameachana na Kajala na ndipo alipojibu kuwa bado wapo pamoja ila hawapendi maisha yao binafsi kuwa katika magazeti kila siku. Quick Racka pia anadaiwa kuwa na tatto yenye jina la Kajala.

Monday, December 7, 2015

Napoleon Asema Lulu Na Wema Sepetu Wana Sifa Za Kufanya Vizuri Hata Hollywood.

Star wa filamu ya Going Bongo inayoendelea kufanya vizuri kimataifa Ernest Napoleon amewataja waigizaji wa Kitanzania Lulu Elizabeth Michael na Wema Sepetu kuwa wana sifa za kufanya vizuri hata Hollywood kama wakipata nafasi na kuwa na management nzuri. Ernest akizungumza na Bongo5 amesema kuwa wengi wanaziponda filamu za Bongo lakini ubovu wa filamu unaweza kusababisha na production mbaya au filamu kutengenezwa ndani ya muda mfupi kwa kuharakishwa lakini suala la uigizaji wa msanii ni kitu kingine.

Sunday, December 6, 2015

Omary Clayton, Timoth Conrad, Filamu Ya Dogo Masai Watamba California Viewers Choice Awards 2015.

Ninaitwa Timoth Conrad Kachumia Director, Producer na Writer wa filamu Tanzania, Ninayofuraha kuwajulisha watanzania kuwa nimefanikiwa kushinda California Viewers Choice Awards 2015, tuzo 2 ikiwa ni Best Feature Film pamoja na Best Director kupitia filamu ya DOGO MASAI, vile vile kutoka katika filamu hiyo hiyo Omary Clayton ambaye ni muigizaji mkuu amefanikiwa kushinda tuzo ya Best Actor.

Saturday, December 5, 2015

Filamu Ya Going Bongo Kuanza Kuonyeshwa Katika Majumba Ya Sinema Nchini Wiki Ijayo.

Filamu ya Kitanzania na ya kimataifa Going Bongo inatarajiwa kuanza kuonyeshwa rasmi kwenye majumba ya sinema nchi kuanzia tarehe 11 mwezi huu wa December. Filamu hiyo iliyochezwa na Ernest Napoleon, Mzee Chilo na wasanii wengine wa kizungu toka mataifa mengine tayari imeshajizolea tuzo katika matamasha kadhaa ya kimataifa na ilianza kuuzwa exclusively katika iTune.

Thursday, November 26, 2015

Wolper Aweka Wazi Jinsi Anavyompenda mchumba Wake.

Muigizaji wa filamu za Bongo, Jacqueline Wolper baada ya kuvalishwa pete ya uchumba na mpenzi wake miezi miwili iliyopita, jana amemwandikia ujumbe mzuri wa siku yake ya kuzaliwa kuonesha jinsi anavyompenda.

Wasanii Wa Filamu Hawana Ubunifu Kama Wasanii Wa Bongofleva: Lulu

MWIGIZAJI wa kike wa filamu aghari Bongo Elizabeth Michael ‘Lulu’ amesema kuwa wasanii wengi wa filamu hawana mawazo ya maana wala kufikiria mambo makubwa kuhusu wanachokifanya bali ufanya tu kwa sababu wapo na jamii inawaona jambo ambalo anahisi Bongo fleva wamewazidi kuwaza.

Picha Odama Alipokutana Na Team Odama Inayomsapoti Katika Kazi Zake.

Hivi Juzi star wa filamu nchini Odama alikutana na watu wa Team Odama ambao humsapoti katika mambo mbalimbali hususani katika kazi zake , hizi ni baadhi ya picha.....

Sunday, November 22, 2015

Shilole Auza Nyumba Aliyokuwa Akijenga Huko Kimara

Msanii Shilole aliwai kuingia kwenye headlines baada ya ku-post kwenye instagram picha ya nyumba yake ambayo alikua bado anaijenga. Caption ya picha hiyo ilikua inasomeka hivi, “Mungu nisaidie nimalize hii kitu ili watoto wangu wasije kupata tabu”.
Eneo ambalo alilokua anajenga nyumba hiyo ni Kimara jijini Dar es Salaam lakini Shilole amesema kwamba ameuza nyumba hiyo ambayo ilikua bado haijaisha vizuri.

JB Anatafuta Script Ya Filamu Acheze Na Mzee Majuto, Changamkia Fursa.

"Tasnia yetu ya filam inakabiliwa na changa moto mbalibali lakini kwangu mimi changa moto kubwa kuliko zote inayo ninyima usingizi ni waandishi wa miswaada(script).
Hili kwangu ndio tatizo kubwa kuliko yote, mfano natarajia kufanya filam yangu na King Majuto, tangu mwaka jana mwezi wa 8 mpaka leo kati ya script 10 nilizoletewa hakuna inayo faa.
Mko wapi waandishi? niko tayari kununua kwa bei yoyote.Lakini ukiniletea kituko tarajia ngumi kama malipo ya usumbufu, ndiyo maana tangu nitoe mzee wa swaga mwezi wa 2 mpaka leo 20-11 sijatoa nyingine...mali ghafi(script) hamna." ameandika JB katika Instagram

Irene Uwoya Arudi Kwenye Filamu Kwa Kishindo Baada Ya Siasa.

Baada ya mikikimikiki ya uchaguzi kuisha, Staa mrembo wa Bongo Movies ambate alikuwa akiwania nasi ya Ubunge kupitia viti maalum , Irene Uwoya amerudi tena kwenye fani yake na sasa yupo kwenye maadalizi ya kazi yake mpya.
Kupitia ukurasa wake kwenye mtandao wa Instagram Uwoya ameandika

Saturday, November 14, 2015

Wolper Kujikita Kwenye Siasa ?

 Jacqueline Wolper Massawe ameweka pembeni masuala ya uigizaji kwa muda usiojulikana kwa kile alichodai ni kujipa muda wa kupumzika na kujikita zaidi kwenye mambo ya siasa.
Rafiki wa karibu na Wolper aliyeomba hifadhi ya jina lake mwanzoni mwa wiki hii, aliliambia gazeti hili kuwa Wolper kwa sasa amekolea sana kwenye mambo ya siasa na kuona kama amekuwa akipoteza muda mwingi kwenye mambo ya uigizaji.

Alichokisema Masanja Baada Ya Kushindwa Kupeta Kura Za Maoni Huko Ludewa.

List ya mastaa wa Bongo Tanzania ambao walijitosa na kujipanga kwenye foleni ya kuusaka Ubunge iliongezeka baada ya mchekeshaji kutoka Kundi la Orijino Komedi, Masanja Mkandamizaji nae kujitosa kwenye foleni hiyo.

Filamu Ya Going Bongo Inahitaji Tuzo Zaidi: Mzee Chilo

Mwigizaji wa filamu, Chilo ametaja sababu tatu zinazoweza kuifanya filamu ya Going Bongo kushinda tuzo zaidi, ambazo ni maandalizi ya muda mrefu, kuona mbali na waigizaji kutambua kazi yao.
Mwigizaji huyo, ambaye jina lake halisi ni Ahmed Olutu, alisema inawezekana mambo mengine yamo ndani ya maandalizi, lakini kiuhalisia kila jambo linajitegemea, kwa sababu unaweza kuandaa kila kitu lakini waigizaji wakawa hawatambui thamani ya ulichokiandaa na kufanya mzaha katika kazi.
Chilo ni miongoni mwa wasanii walioigiza kwenye filamu ya Going Bongo iliyoshirikisha waigizaji kutoka nchi sita na ambayo imejishindia tuzo kadhaa.

Monday, November 9, 2015

Tasnia Ya Filamu Nchini Imeyumba Mwaka Huu: Johari.

Muigizaji wa filamu, Johari Chaula amesema kuwa mwaka 2015 haukuwa mzuri kwa wasanii wa filamu.
Johari ameiambia Bongo5 kuwa wasambazaji wa filamu wamezidiwa na kazi zinazozalishwa na wasanii.
“Mwaka huu si mzuri sana kiukweli kwa sababu wasanii wa filamu wamekuwa wengi na tunazalisha sana filamu mpaka wasambazaji wanazishindwa na wao wanasema soko haliko vizuri,” amesema.

Wema Na Diamond Walipuana

BAADA ya muigizaji nyota Wema Sepetu ‘kumtusi’ mpenziwe wa zamani, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, kwa kudhihaki zawadi ya bei chee ya gari aliyowahi kumnunulia, rais huyo wa lebo ya Wasafi Classic Baby (WCB), juzikati aliibuka na kumjibu kuwa amefanya mambo ya ‘Kiswahili’.
Akizungumza ofisini kwake Sinza Mori jijini Dar es Salaam, Diamond alisema katika maisha kila mmoja ana ndoto zake, hivyo ni jambo jema kwamba amefanikisha, lakini hata hivyo, akasema hatua aliyofikia yeye siyo ya kufanya mashindano na mtu, badala yake ni kuchapa kazi kusaka mafanikio zaidi ya maisha yake.

Lulu Awambwatukia Wanaohoji Urembo Wake.

STAA asiyekaukiwa matukio Bongo Movies, Elizabeth Michael ‘Lulu’ amewacharukia watu wanaohoji kwa nini anapendeza angali mwanafunzi kwa kuwaambia, ‘kwani akiwa mwanafunzi ni mwiko kupendeza?’
Akizungumza  na mwandishi wa habari hii hivi karibuni,  Lulu alisema amekuwa akiona maoni ya watu wengi mtandaoni wakihoji anapata wapi fedha za kupendeza wakati yeye ni mwanafunzi hoja ambayo ameiona haina mashiko kwani yeye hatumii fedha nyingi katika urembo wake.

Wednesday, November 4, 2015

Nilitamani Diamond Platnumz Awe Mume Wangu: Wema Sepetu

Jina la Nasib Abdul bado halijatoka kichwani mwa Wema Sepetu!
Nasib Abdul ni jina halisi la Diamond Platnumz.
Miss Tanzania huyo wa mwaka 2006 na muigizaji wa filamu alikuwa akijibu swali kwenye kipindi cha Hitzone kupitia kituo cha redio cha Jembe FM cha jijini Mwanza alipoulizwa ni mwanaume gani ambaye alitamani awe mume wake wa ndoa.

Mume Asema Bado Anampenda Shamsa Ford.

ALIYEKUWA mzazi mwenziye na staa wa filamu Bongo, Shamsa Ford, Dickson Matoke amesema kuwa ndani ya moyo wake bado anampenda sana na kumthamini mkewe huyo kama mama wa mtoto wake siku zote za maisha yake.

Faiza Ally Kuja Na Filamu Ya Baby Mama Drama.

Baada ya kushambuliwa na baadhi ya watu kuhusu malezi ya mtoto wake Sasha, aliyekuwa mke wa zamani wa Sugu, Faiza Ally ameamua kuweka wazi mpango wake wa kuachia filamu iitwayo ‘Baby Mama Drama’.

Tuesday, November 3, 2015

Picha Kutoka Royal Birthday Ya Wema Sepetu.

Wema Sepetu alianda party ya birthday yake iliyohudhuriwa na masataa na watu wake wa karibu. Hizi ni picha.......

Sitaacha Muziki Licha Kuchaguliwa Kuwa Mbunge Wa Mikumi. Professor Jay

Joseph Haule "Prefessor Jay" amabye ni msanii maarufu wa hip hop nchini amesema kuwa hataacha muziki hata kama amechaguliwa kuwa mbunge wa jimbo la Mikumi. Professor Jay alisema kuwa muziki ndio umefasnya wengi wamjue yeye na harakati zake za kuipigania jamii. Hivyo atawatumikia wananchi wa jimbo la Mikumi kuleta maendeleo lakini pia muziki atafanya kama kawaida kufikisha ujumbe kwa jamii.

Magufuli Awashukuru Wasanii Kwa Kumpigia Kampeni.

HAIKUWA kazi rahisi katika kuusaka urais kwa awamu ya tano kila chama kilitumia mbinu katika kuhakikisha kinaibuka kidedea, na hatimaye Dr. John J Pombe Magufuli kuteuliwa kuwa rais wa awamu ya tano, mh. Rais mteule amewashukru wasanii kwa support yao wakati wa kampeni.

Saturday, October 31, 2015

Wala Sijapotea Nipo Najipanga.

MWIGIZAJI wa kike katika tasnia ya filamu Bongo Nuru Nassor ‘Nora’ anasema hajapotea katika tasnia ya filamu bali ni kujipanga na kufanya kazi zake zaidi kuliko za kushirikishwa kwani mara nyingi filamu ili ung’are lazima uwe mtayarishaji.

Davina Ahamasika Kugombea Ubunge Uchaguzi Ujao.

HALIMA Yahya ‘Davina’ amehamasika na mambo ya kisiasa hivyo, kujiandaa kwa kujifua vyema kwa ajili ya msimu ujao wa uchaguzi (2020).
Akizungumza na paparazi wetu hivi karibuni, Davina ambaye ni msanii wa filamu Bongo, alisema kufuatia kupata fursa ya kushiriki kampeni kwa nafasi yake, maeneo mbalimbali ya nchi, amejikuta akishawishika kuwa kiongozi na kwamba baada ya miaka mitano, endapo Mungu atamjaalia uzima, atagombea nafasi ya ubunge, mkoani Iringa.

Dr.Cheni Aiomba Serikali Ya Magufuli Kutimiza Ahadi Ya Wasanii Kufaidika Na Kazi Zao.

Mahsein Awadh Said ‘Dk Cheni’ hivi karibuni ametoa ya moyoni kwa kusema kuwa serikali
ijayo iache mambo ya blabla bali itimize ahadi ambazo imekuwa ikitoa kwa wasanii ikiwa ni pamoja na kulinda haki
na masilahi yao.

Saturday, October 24, 2015

Kifo Cha Deo Filikunjombe Kimenihuzunisha Sana: Cathy Rupia

Muigizaji wa muda mrefu, Sabrina Rupia ‘Cath wa Mambo Hayo’,  amekiri kuumia vibaya kufuatia kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Ludewa, Deo Filikunjombe kutokana na ukaribu wao na jinsi alivyokuwa na moyo wa kuwajali wengine.
Akizungumza kwa uchungu na mwandishi wetu kwa njia ya simu kutoka Ludewa alikohudhuria mazishi ya mbunge huyo, Cath alisema maumivu aliyonayo kamwe hayasimuliki na kwamba itamchukua muda mrefu kumsahau Deo na kwamba ataendelea kumuombea kwa Mungu, ampumzishe kwa amani.